DVD YA MUNGU HABADILIKI YA MESS JACOB CHENGULA

Tuesday, January 28, 2014

DANCER WA BONY MWAITEGE, CLAUDY P. MWAKALASYA ASHUHUDIA MAISHA YAKE

Claudy P. Mwakalyasa ni mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania. Kabla ya uimbaji alikuwa dancer wa mwimbaji maarufu sana Tanzania, Bony Mwaitege. Amekuwa naye kwa muda mrefu sana kwa kazi ya Mungu. Claudy Mwakalyasa siku ya jana aliweza kuongea na Rumafrika ambapo aliweza kuzungumzia maisha yake kabla ya kuokoka na baada ya kuokoka. Claud moja ya sifa aliyokuwa nayo kabla ya kumpokea Yesu Kristo kuwa mwokozi wa maisha yake, alikuwa ni mtu wa pombe sana hasa kilevi cha ulanzi. Baada ya kusikia huduma ya Bony Mwaitege aliamua kumfuatilia ili aweze kufanya naye kazi. Juhudi za Claud P. Mwakalyasa ziliweza kuleta matunda na baadae akaweza kumpata Bony Mwaitege na kuwa dancer wake.

Claudy P. Mwakalasya


Kuna mengi Claudy Mwakalyasa aliweza kufunguka juu ya maisha yake kabla ya wokovu na baada ya wokovu, njia alizotumia kumpata Bony Mwaitege ikiwa ni pamoja na kuomba vazi la Bony alivae ili apata kuwa kama Bony Mwaitege kwa kuimba, matatizo mbalimbali aliyopambana nayo katika huduma yake ya kucheza, sababu zilizomfanya aachane na ku-dance na Bony Mwaitege na kusimama kama mwimbaji, nini anazungumzia juu ya waimbaji wengine wa nyimbo za injili. Endelea kufuatilia habari zake kwa kupitia blogu yetu hii.

Unaweza kuwasiliana naye kwa simu +255 756 573 788 au +255 712 616 112

MUNGU WANGU WA MBINGUNI NA AKUBARIKI.

Source: RumAfrica
www.rumaafrica.blogspot.com

No comments:

Post a Comment