DVD YA MUNGU HABADILIKI YA MESS JACOB CHENGULA

Sunday, June 29, 2014

TAIYA ODERO (SUZY) AMCHANGANYA BOSS WAKE KIMAPENZI OFISINI

Ile filamu iliyokuwa ikisubiriwa na watu wengi sana duniani ya INSIDE ya Jennifer Kyaka (Odama) cnini ya kampuni ya J-FILM 4 LIFE sasa itakuwa sokoni 10.07.2014. Utaweza kuona vituko vya maofisini kati ya wafanyakazi na mabosi. Taiya Odero (Suzy) ataona anavyofanya vitu vyake dhidi ya boss wa kampuni akitaka mapene kwa kupitia mapenzi na baadae kujutia tabia yake.

Filamu hii inawafundisha hata waliokoka ambao wokovu wao haujasimama na wanatumia wokovu kufanya vitendo viovu na wakubwa wao wa kazi wakitaka kujipatia pesa. Wanatumia uzuri wao kuwadanganya mabosi wao na mwisho wa siku wanajikuta wanaingia katika matatizo makubwa.

Kwahiyo kwa kupitia filamu hii utaweza kufunguka na kujifunza mengi


KANISA LA YESU KRISTO LA WATAKATIFU WA SIKU YA MWISHO WAKARIBISHA WATU MBALIMBALI KATIKA KANISA


Kiongozi wa shule ya jumapili wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za mwisho,Dr, Emanuel Kandusi akiwapatia maelezo mbalimbali kwa watu waliotembelea kanisa hilo wakati wa siku ya wazi kwa ajili ya watu mbalimbali kuangalia shughuli zinazofanywa na kanisa hilo


Baadhi ya watu waliotembelea kanisa hili wakipata maelekezo mbalimbali


Mwakilishi wa Darasa la Mkono msaidizi wa akina mama Happy Ayubu akitoa maelezo kwa watu waliotembelea kanisa hilo


Baadhi ya watu waliotembelea kanisa hili wakipata maelekezo mbalimbali
Mhumini waKanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za mwisho Framers Ngosha akijibu maswali ya watu waliojitokeza katika siku hiyo
Kiongozi wa shule ya jumapili wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za mwisho,Dr, Emanuel Kandusi 'kulia' akionesha vitabu vinavyotumika kwa ajili ya mafunzo kushoto ni Rais wa tawi la Mbezi Beach, Malabi Kyubi


Rais wa tawi la Mbezi Beach, Malabi Kyubi akitoa maelezo

Baadhi ya watu mbalimbali waliotembelea katika kanisa hilo lililopo Mbezi Beach

Baadhi ya watoto wa waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za mwisho wakicheza na kuimba wakati wa siku ya wazi kwa watu kutembelea na kuona mambo mbalimbali iliyofanyika katika kanisa lao la Mbezi Beach jijini Dar es salaam

Baadhi ya watoto wa waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za mwisho wakicheza na kuimba wakati wa siku ya wazi kwa watu kutembelea na kuona mambo mbalimbali iliyofanyika katika kanisa lao la Mbezi Beach jijini Dar es salaam

Baadhi ya watoto wa waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za mwisho wakicheza na kuimba wakati wa siku ya wazi kwa watu kutembelea na kuona mambo mbalimbali iliyofanyika katika kanisa lao la Mbezi Beach jijini Dar es salaam

watu waliotembelea wakipata mahelezo mbalimbali

Baadhi ya watu waliotembelea katisa hilo

PICHA: MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI ROSE MUSHI APATA MUME MWEMA.

Duniani wawili wawili, hili limetimia kwa mwimbaji wa nyimbo za Injili Rose Mushi baada ya kiu yake ya kuwa na mume kukausha siku ya leo ikishuhudiwa na mama mchungaji Maboya ambaye alimtoa rasmi kwaajili ya kukutana na mume wake kipenzi. Tutazidi kuwaletea mengi juu ya harusi hiii


Rose Mushi na mumewe.
 Mama Mchungaji Maboya Mchungaji wa Rose akimtoa rasmi kuweza kuolewa

TAIYA ODERO (SUZY) AMCHANGANYA BOSS WAKE KIMAPENZI OFISINI

Ile filamu iliyokuwa ikisubiriwa na watu wengi sana duniani ya INSIDE ya Jennifer Kyaka (Odama) cnini ya kampuni ya J-FILM 4 LIFE sasa itakuwa sokoni 10.07.2014. Utaweza kuona vituko vya maofisini kati ya wafanyakazi na mabosi. Taiya Odero (Suzy) ataona anavyofanya vitu vyake dhidi ya boss wa kampuni akitaka mapene kwa kupitia mapenzi na baadae kujutia tabia yake.

Filamu hii inawafundisha hata waliokoka ambao wokovu wao haujasimama na wanatumia wokovu kufanya vitendo viovu na wakubwa wao wa kazi wakitaka kujipatia pesa. Wanatumia uzuri wao kuwadanganya mabosi wao na mwisho wa siku wanajikuta wanaingia katika matatizo makubwa.

Kwahiyo kwa kupitia filamu hii utaweza kufunguka na kujifunza mengi


Saturday, June 28, 2014

VUNJA MBAVU NA VITUKO VYA MAOFISINI KATIKA FILAMU YA INSIDE. IPO SOKONI KUANZIA 10.07.2014

Filamu hii Jennifer Kyaka (Odama) ambayo inayonyesha maisha ya wafanyakazi maofisi wanaovyofanya vituko na mabosi wao na wengine hata kumkufuru na kumuudhi Mungu kwa vitendo vya rushwa na uvivu kazini, kwa mana Mungu amesema asiyefanya kazi na asile. Watu badala ya kufanya kazi wanabaki kupiga stori na majungu maofisi. Wadada wanavyotumia uzuri wao kuwalaghai waume za watu kwa kutoa rushwa ya ngono. Hakika kama mcha Mungu ndani ya hii filamu utajifunza mengi na utaburudika na vituko vya wasanii maarufu wa kuchekesha kama KING MAJUTO na  BENY, pia utamuona marehemu RACHEL HAULE, DAVINA, ODAMA, DULLAH WA PLANET BONGO, na wengine wemgi sana. Filamu hii ambayo imetengezwa na kampuni bora Tanzania ya J-FILM 4 LIFE itakuweka mahali fulani KIMAWAZO.

BW. EMMANUEL MBASHA NA FLORA MBASHA WAPATANA

HAKUNA neno zuri la kusema zaidi ya Mungu mkubwa! Ule mtafaruku ndani ya ndoa ya mwimba Injili mahiri Bongo, Flora na mumewe, Emmanuel Mbasha umedaiwa kumalizika kwa wawili hao kupatana, Risasi Jumamosi linakuwa nambari wani kukuhabarisha.

Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika, wawili hao walikalishwa kikao cha upatanishi mapema wiki hii kilichokuwa chini ya familia.

Flora Mbasha akiwa kwenye picha ya pamoja na mumewe, Emmanuel Mbasha.

MANENO YA CHANZO
“Kikao cha familia kilikaa, Mbasha aliitwa akafika, Flora naye aliitwa akatokea, mazungumzo yalikuwa marefu lakini kimsingi waliamua kuweka kando mtafaruku wao na kuijenga upya ndoa yao,” kilisema chanzo.

Chanzo kiliongeza kuwa katika kikao hicho cha mwanzoni mwa wiki hii, miongoni mwa adidu za rejea ilikuwa kutokumbushia vikao vilivyopita ambapo hakukupatikana muafaka.

VIKAO VILIVYOPITA
Katika vikao vilivyopita, wahusika wakuu walikuwa wazazi wa Mbasha (mzee Maneno Mbasha, Zulfa Maneno), ndugu wa Flora na Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.


Mwimbaji Injili mahiri Bongo, Flora Mbasha.

VIKAO VYA BAADAYE
Kwa mujibu wa chanzo, vikao vilivyofuata, wawili hao wakawa tayari kila mmoja ametema nyongo yake pembeni na kufikia makubaliano kwamba, ndoa yao isimame tena wakitumia maandiko kwenye Biblia kutoka kitabu cha Waebrania yanayosema: Ndoa na iheshimiwe na watu wote na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.

WAKORINTHO YAFUNGA KAZI
Kwa mujibu wa chanzo hicho, maneno mengine ya Biblia yaliyotumika kwenye kikao hicho mpaka wawili hao wakaamua kurudiana ni 1 Wakorintho 7:1-10 ambapo maandiko yanasema:
Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe. Mume na ampe mkewe haki yake vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

Mke hana amri juu ya mwili wake bali mumewe vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake bali mkewe. Msinyimane, isipokuwa mmepatana kwa muda ili mpate faragha kwa kusali, mkajiane tena shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.

Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza, wala hapo si mimi, ila Bwana (Mungu), mke asiachane na mumewe, lakini ikiwa ameachana naye na akae asiolewe au apatane na mumewe, tena mume asimwache mkewe.

KIKAO CHA JUMAMOSI KUMALIZIA
Chanzo kilisema kuwa, kikao cha mwisho ambacho kitamalizia kuweka mambo sawa ili wawili hao waanze ngwe ya pili ya ndoa yao ambayo inaaminika itakuwa ya mwisho mpaka kifo kiwatenganishe, kinatarajiwa kufanyika leo jijini Dar es Salaam mahali ambapo hapakutajwa.

Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.

MWANASHERIA ATAJWA
Mwanasheria wa Flora aliyejulikana kwa jina moja la Addo Novembaer ametajwa kusimamia kikao hicho ili wawili hao waanze maisha mapya baada ya safari fupi ya mvurugano uliowafanya kuwa mbalimbali.

AONGEA NA RISASI JUMAMOSI
Juzi, Risasi Jumamosi lilimsaka mwanasheria huyo kwa njia ya simu yake ya mkononi ili kumsikia anasemaje kuhusu kutajwa kwenye usuluhishi wa ndoa hiyo ambapo alipopatikana alisema:
“Niko Arusha, Ijumaa nitarudi Dar. Kuhusu kikao cha usuluhishi siwezi kukwambia lakini suala la kuwapatanisha nalifahamu, nawaomba na ninyi msaidie kufanikisha jambo hilo zuri.”

VIPI KUHUSU KESI YA MADAI YA KUBAKA?
Hata hivyo, Wakili Ado hakutaka kugusia kuhusu kesi ya Mbasha iliyopo Mahakama ya Wilaya ya Ilala ambapo anadaiwa kumbaka shemejiye mara mbili (jina tunalo) ambayo kwa mujibu wa mahakama, upelelezi umekamilika na itasikilizwa Julai 17, mwaka huu.

KWA UPANDE WAKE FLORA
Risasi Jumamosi lilimwendea hewani, Flora ili kumsikia anasemaje kuhusu kuwepo kwa upatanishi kati yake na mumewe, Emmanuel.

Huyu hapa: “Ongea na wakili wangu atakwambia kila kitu.” Ambapo majibu ya wakili yalikuwa: ”Ninachojua mimi ni kwamba Flora ameshamsamehe mumewe na yuko tayari kuanza ukurasa mpya.”

MBASHA SASA
Kwa upande wake, Mbasha alipozungumza na gazeti hili juzi alisema kurejea upya kwa ndoa yake ni jambo la kuupendeza moyo wake.

“Mimi sina neno nipo tayari, nimeshasamehe yaliyotokea, Flora ni mke wangu jamani, nampenda sana kutoka moyoni.”

VIONGOZI WA DINI WAJA VIKALI JUU YA STAA WA BONGO MUVI J. WOLPER KUBADILIBADILI DINI

Stori:Gladness Mallya
TABIA ya staa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper kubadilibadili dini mara kwa mara imeonekana kuwakera watu mbalimbali akiwemo Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa Salum ambaye amemcharukia vikali.


Staa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper akipozi.

Wolper kiimani ni Mkristo lakini hivi karibuni alibadili na kuwa Muislam kabla ya kurejea tena kwenye imani yake ya awali ya ukristo.

Sababu ya Wolper kubadili dini ilikuwa ni kufunga ndoa na aliyekuwa mchumba wake Abdallah Mtoro ‘Dalas’, walipoachana akaamua kurudi kwenye ukristo.

Akizungumza na Risasi Jumamosi juzikati, Shehe Salum, alisema Wolper anapaswa kujichunguza na kubadilika haraka kwani kitendo anachofanya ni kinyume na taratibu za dini.
“Siyo vizuri hata kidogo na hata dini zote zinakemea kitendo cha kuchezeachezea dini kwani ni chukizo kwa Mungu.


Jacqueline Wolper akiwa kazini.

“Kwa upande wa Dini ya Kiislamu, kuna sheria kali zaidi kwa mtu akionekana na tabia hiyo, anaweza hata kuuawa hivyo wanaofanya mchezo huo waache kwani siyo vizuri. Huko ni kumfanyia Mungu dhihaka,” alisema Shehe Salum na kuongeza:

“Unajua suala la imani ni kitu kinachomhusu mtu binafsi, ni vyema kufanya uamuzi wa hakika na kushika njia moja na siyo kufanya dhihaka na dini ya Mwenyezi Mungu. Ni kitu kibaya sana.”
Naye Juma Suleiman, mkazi wa Ilala, jijini Dar es Salaam alimwambia mwandishi wetu kuwa, katika imani ya kiislam kunakatazwa watu kucheza na dini huku akisisitiza anayefanya hivyo anaweza kulaaniwa.

“Dini siyo kitu cha kuchezea, ni daraja la kumfikisha mtu kwenye haki, si mahala pa kuingia na kutoka, kuingia na kutoka. Huko ni kucheza na Mungu. Namshauri huyo mtoto (akimaanisha Wolper) abadilike. Asifanye mchezo na imani, Mungu anaweza kumlaani kwa kumchezea,” alisema Suleiman.

Friday, June 27, 2014

MFULULIZO WA MBEYA GOSPEL FESTIVAL: ANN ANNIE, RACHEL, MESS JACOB CHENGULA NA WAIMBAJI WENGINE WATIKISA MBEYA

Chama cha Muziki wa Injili Tanzania kiliandaa tamasha linaloenda kwa jina la Mbeya Gospel Festival likiwa na lengo la kuwataka wana Mbeya kujiunga na chama hicho kwaajili ya kuwasaidia kujua haki zao za kimuziki.

Katika tamasha hili kulikuwa na waimbaji wengi sana kama vile Mess Jacob Chengula, Ann Annie, Rachel, na wengine wengi. Watu walibarikiwa sana.

 Kutoka kulia ni Rachel, Ann Annie
 Rachel Sharp kutoka Sweden
 Emmanuel Mabisa

 Mess jacob Chengula mwenye koti jeupe

Ann Annie

MZEE WA KANISA ANASWA LIVE GESTI NA BINTI CHINI YA MIAKA 18...MATUKIO KATIKA PICHA



Mzee wa kanisa la kiroho (jina linahifadhiwa kwa sasa), aliyetajwa kwa jina la Luca Pesa, mkazi wa Segerea, Dar, ameaibika baada ya kukurupushwa kwenye nyumba ya kulala wageni (gesti) akidaiwa kutaka kuvunja amri ya sita na binti ambaye ni msanii chipukizi wa filamu za Kibongo, Debora Jacob, Ijumaa lina kisanga cha aina yake.


Mzee wa kanisa la kiroho aliyetajwa kwa jina la Luca Pesa,

HABARI KAMILI
Tukio hilo ambalo kamwe Luca hawezi kulisahahu maishani mwake, lilijiri kwenye gesti hiyo iliyopo karibu na Kituo Kikuu cha Mabasi cha Segerea, Dar, Jumanne iliyopita huku mzee huyo akishushiwa tuhuma nzito ya rushwa ya ngono kwa vibinti chini ya miaka 18.
Katika tukio hilo, mzee huyo wa kanisa na msanii huyo wa Kundi la Maigizo la Vivif lenye maskani yake maeneo hayo walikuwa wamejichimbia kwenye gesti hiyo katika chumba ambacho mlangoni kilikuwa kimeandikwa Rombo kabla ya kuchomolewa na kufikishwa kanisani kisha polisi.

TUHUMA NZITO
Timu ya Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers, ikiwa kwenye mingo zake, ilipokea simu kutoka kwa dada aliyejitambulisha kwa jina moja la Diana na kujieleza kuwa anatoka kundi la sanaa za maigizo la Vivif lililopo Segerea jijini Dar.
OFM: Ndiyo hujakosea unazungumza na
OFM, tukusaidie nini?
Diana: Kuna mzee wa kanisa la kiroho la (anataja jina la kanisa hilo) lililopo maeneo ya Segerea, aliomba kuwa mfadhili wa kundi letu.

Akiwa kwenye geti la kanisa.

Tulimkubalia na baada ya muda alianza kutumia fedha zake vibaya kwa kufanya vitendo visivyofaa.
OFM: Vitendo gani visivyofaa?
Diana: Anawarubuni mabinti wadogo anawaweka kambini na kula nao tunda tamtam eti ndiyo tiketi ya kuchezeshwa kwenye maigizo.
OFM: Tiririka!
Diana: Yaani hadi muda huu ninapozungumza na ninyi mzee huyo wa kanisa anachati na msanii mwingine wa kundi hilo. Anaitwa Debora anataka waende kwenye gesti fulani wakanogeshane, wahini tayari mtego umewekwa utafyatuka muda wowote.

UDHALILISHWAJI?
Diana alisema baada ya Debora kuombwa ‘mambo’ ndipo akawataarifu wasanii wenzake na kuwataka wote kwa pamoja waungane kuikomesha tabia hiyo chafu ya Luca anayelichafua kanisa la kiroho na kulidhalilisha kundi lao la sanaa.

OFM MZIGONI
Baada ya kuseti kila kitu, Diana aliiomba OFM iambatane nao kwani muda huo tayari Debora alishatangulia kwenye gesti hiyo kumfuata mzee huyo wa kanisa ambaye alishachukua chumba.

.....akitaitiwa.

Taarifa hiyo ilipokelewa kwa mikono miwili na kiongozi wa OFM ambaye aliwaagiza vijana wake makini ambao walisitisha kazi nyingine za kiintelijensia kisha kuelekeza nguvu zao eneo la tukio.
Vijana hao walitumia pikipiki zao ziendazo kasi ambapo baada ya muda usiozidi dakika ishirini walikuwa wamefika kwenye gesti hiyo.

ENEO LA TUKIO
OFM walipofika eneo la tukio, walikuta kundi la wasanii hao wakimchomoa gesti mzee huyo wa kanisa ambaye aliruka ukuta na kudondokea kwenye matuta ya viazi.
Akiwa anajizoazoa kwenye matuta hayo, kundi la wasanii hao lilimuunganishia ambapo kabla ya kumnasa aliingia kwenye chumba cha nyumba iliyopo jirani na gesti hiyo ili kujisalimisha.
Hata hivyo, zoezi lake lilifeli baada ya wasanii hao kumtahadhalisha mwenye nyumba hiyo kuwa wanamtaka mtuhumiwa wao la sivyo wangeichoma moto.
Baada ya kuzingirwa na wasanii hao huku akihatarisha maisha yake kwa kuwa wasanii hao walikuwa na hasira, aliona yasiwe makuu akaamua kuwaruhusu wamtoe mtuhumiwa wao wakamalizane naye kanisani.

KABANG!
Alipotiwa mikononi, mzee huyo wa kanisa aliomba apelekwe kanisani ambapo hapakuwa mbali na eneo la tukio ili akahifadhi vitu vyake muhimu pamoja na kuomba ushauri.

APELEKWA MSOBEMSOBE KANISANI
Kundi hilo la wasanii lilimpeleka kanisani msobemsobe ambapo baada ya hatua kadhaa polisi walitokea na kuwadhibiti wananchi wenye hasira na wasanii waliotaka kumdhuru mzee huyo wa kanisa wakati akipelekwa kanisani.

Mtuhumiwa akitembezwa mtaani.

MTAANI WERAAA!
Wakiwa mitaani, njiani mabinti walikuwa wakipiga kelele ‘weraaa…ukomeee…’ huku wakifurahia kufunga mitaa kwa madai kwamba mzee huyo wa kanisa alizidi.
Katika sekeseke hilo, polisi hao walimtia pingu mzee huyo wa kanisa na kuongoza safari ya kuelekea kanisani.
Wakiwa kanisani hapo polisi walijitambulisha na kuwauliza wachungaji pamoja na waumini wa kanisa hilo kama walimfahamu mzee huyo wa kanisa.

BREKI YA KWANZA POLISI
Kundi la wazee pamoja na vijana wa kanisa hilo walikiri kuwa Luca ni mmoja wa wazee wa kanisa hilo ndipo polisi hao wakamruhusu kuwakabidhi baadhi ya vitu vyake ikiwemo simu na fedha kisha breki ya kwanza ikawa Kituo cha Polisi cha Tabata-Shule ambapo alifunguliwa jalada la kesi namba RB/3843/2014 -RUSHWA YA NGONO, KUWAWEKA KAMBI KINYUME CHA SHERIA WASICHANA WENYE UMRI CHINI YA MIAKA 18 NA KUWADHALILISHA KIJINSIA.
Hadi OFM wanaanua jamvi kituoni hapo kanisa lilikuwa likihaha kumchomoa kwa dhamana akisubiri sheria kuchukua mkondo wake.

Source: Vituko vya mtaa

Wednesday, June 25, 2014

UNAPENDA KUCHEKA NA KUJUA VITUKO VYA MAOFISINI...JIPATIE NAKALA YAKO YA INSIDE YA ODAMA KUTOKA J FILM FOR LIFE

Sasa ile filamu iliyokuwa ikisubiliwa na Watanzania wengi ya INSIDE kutoka kwa Jennifer Kyaka (Odama) itakuwepo sokoni 10.07.2014. Filamu hii ambayo imechezwa katika  mazingira ya ofisini ikionyesha vituko vinavyofanyika maofisi na wafanyakazi na pia mabosi. Kama kawaida ya kampuni ya J-Film 4 Life ndio iliyohusika katika kutengeneza filamu hii ambayo ukiangalia utavutiwa na kujua mengi kuhusiana na vituko vya vinatokea  maofisini

Ndani ya filamu hii kuna vituko vya ajabu ukisingatia yumo Majuto, Beny, Dullah, marehemu Rachel Haule, Odama na wengine wengi kama unavyoona katika cover. Jipange mtu wangu kujipatia hii nakala ambayo mpya upate kuongeza siku zako za kuishi kwa kicheko.

Tembelea
www.odama1.blogspot.com


MKURUGENZI WA HOTELI YA TUGIMBE MBEYA ATOA OFA YA CHAKULA KWA WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI WALIOSHIRIKI MBEYA GOSPEL FESTIVAL 2014

Waimbaji wa nyimbo za injili Tanzania waliweza kujipatia ofa ya chakula katika hotel maarufu mkoani Mbeya ya Tugimbe baada ya kufanya kazi ya Mungu katika lile tamasha kubwa lililoandaliwa na Chama Cha Muziki wa Injili Tanzania (CHAMUITA) mkoani Mbeya linaloenda kwa jina la Mbeya Gospel Festival. Mkurugenzi Fadhili Ngajilo aliguswa sana na huduma ambayo ilileta uvuvio mkubwa sana kwa wakazi wa Mbeya na watu waliweza kuokoka na wengine kuvutiwa kuwa waimbaji

Tamasha hili lililenga kuwataka wakazi wa Mbeya kujiunga na chama hiki ili waweze kujua haki zao na chama kulinda haki zao za muziki wa Injili Tanzania





MESS JACOB CHENGULA NA EMMANUEL MABISA KATIKA CAMP YA VIJANA MKOANI IRINGA

Baada ya kazi nzito mkoani Mbeya katika Mbeya Gospel Festival, Emaanuel Mabisa na Mess Jacob Chengula waliweza kumtangaza Yesu Kristo kwa njia ya uimbaji katika Camp ya vijana wa Pentekostal Holiness iliyofanyika katika chuo cha Kileluu mkoani Iringa.
Mess Jacob Chengula

Hii inapendeza sana kuona vijana wanaacha kazi zao na kupoteza muda kwa kazi ya Mungu. Vijana wengi tuko busy sana kwa kazi za duniani na tunatumia muda mdogo sana kwa kazi ya Mungu. Tunapokuwa na shida tunamtafuta sana Mungu lakini tukiwa katika starehe tunamsahau Mungu Baba. Mess Jacob Chengula na Emmanuel Mabisa wameliona hilo na ndio maana wameamua kumtumikia Mungu wakati wa ujana wao.

Emmanuel Mabisa

Tukumbuke siku ya mwisho Mungu wetu atatuuliza tulifanya nini wakati tupo duniani, tutatoa hesabu zetu. Hujachelewa kijana mwenzangu, amua sasa kufanya kazi ya Mungu kama punda kwa kuhubiri injili ya Yesu Kristo na kuwaleta watu kwa Yesu Kristo. Tuache kujiona mastaa na kuionea aibu injili ya Yesu.

Kila mtu hapa duniani amepewa kazi ya kufanya kwaajili ya utukufu wa Mungu. Muulize Mungu wako nini cha kufanya kwaajili yake naye atakujibu na kukupa kazi ya kufanya. Nadhani unajua ya kwamba kama hutafanya kazi ya Mungu na ukaamua kumtumikia shetani, basi siku ile ya mwisho utatupwa jehanamu ukiungua kwa moto mkali sana.

Watumishi wa Mungu hubiri injili ya kuwapeleka watu kwa Mungu, na tuache kuhubiri ili watu wajae kanisani na tupate sadaka nyingi. Huu ni wakati wa kumtumikia Mungu wetu. Watumishi wa Mungu fikeni vijijini kwani huko watu wanateseka sana na wanakosa watu wa kuwainua kiimani. Wamezungukwa na mapepo, majini, wachawi na wamekuwa wafungwa wa kiroho

Wenu katika Bwana
Rulea Sanga
RUMAFRICA FOR ALL NATIONS


 Emmanuel Mabisa
 Mess Jacob Chengula

 Emmanuel Mabisa



 Emmanuel Mabisa